Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

ANGALIA PICHA_KIKAO CHA UHAMASISHAJI WA MASUALA YA LISHE KWA VIONGOZI WA MKOA NA WILAYA SHINYANGA

Taasisi ya Chakula na Lishe nchini kwa kushirikiana na  ofisi ya mganga mkuu mkoa wa Shinyanga jana Aprili 22,2015 wamefanya kikao cha Uhamasishaji wa Masuala ya Lishe kwa viongozi wa mkoa wa Wilaya iliyofanyika katika ukumbi wa Empire Mult Hotel mjini Shinyanga-Picha zote na Kadama Malunde-Shinyanga

Lengo la kikao hicho ni kuwapatia viongozi hamasa katika kupambana na matatizo ya Lishe Duni inayoathiri afya na maendeleo katika mkoa ikiwa ni pamoja na wanafunzi kutofanya vizuri darasani na kuongeza maradhi na vifo hasa kwa watoto wa umri chini ya miaka mitano na wanawake walio katika umri wa kuzaa.
Kulia ni Mkurugenzi wa taasisi ya Chakula na Lishe nchini Tanzania Dr Joyceline Kaganda akizungumza katika kikao hicho ambapo alisema takwimu za lishe mkoa wa Shinyanga mwa ka 2014 zinaonesha kuwa asilimia 30 ya watoto wamedumaa ukilinganisha na mwaka 2010 ambapo asilimia 43 ya watoto walikuwa wamedumaa huku wilaya ya Kishapu ikiongoza ikifuatiwa na wilaya ya Shinyanga,Ushetu,Msalala,Shinyanga manispaa na Kahama mji.Kushoto kwake ni kaimu mganga mkuu mkoa wa Shinyanga Dr Fabian Kalabwe kwa niaba ya katibu tawala mkoa wa Shinyanga.
Wajumbe wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea kwenye  kikao 

 Mkurugenzi wa taasisi ya Chakula na Lishe nchini Tanzania Dr Joyceline Kaganda akizungumza katika kikao hicho
Waandishi wa habari wakiwa ukumbini 
Kaimu mganga mkuu mkoa wa Shinyanga Dr Fabian Kalabwe kwa niaba ya katibu tawala mkoa wa Shinyanga akitoa hotuba ambapo alizitaka halmashauri za wilaya na mkoa kujumisha shughuli za lishe na kupewa kipaumbele katika mipango yao huku akizitaka halmashauri ambazo bado zinatumia waratibu wa lishe wasio na sifa waache mara moja kwani watakosa fursa nyingi hasa miradi inayosimamiwa na wahisani.

Mwezeshaji wa kitaifa kwa viongozi ngazi za mikoa na wilaya ambaye pia ni Afisa Lishe mkoa wa Iringa Mwita Waibe akitoa mada ambapo alisema miongoni mwa nchi zinaongoza kwa utapiamlo barani Afrika ya Kwanza ni Ethiopia,ya pili DRC,Tanzania inachukua nafasi ya tatu.

Kikao kinaendelea

Mwezeshaji wa kitaifa kwa viongozi ngazi za mikoa na wilaya ambaye pia ni Afisa Lishe mkoa wa Iringa Mwita Waibe alitaka elimu itolewe kwa wananchi juu ya umuhimu wa lishe kwa watoto ndani ya siku 1000 ili kuwaepusha na udumavu.Alisema katika mkoa wa Shinyanga kati ya watoto 100,30 wamedumaa hivyo kuitaka jamii kuwapa watoto vyakula vyenye madini joto ili kujenga ubongo wao-Picha zote na Kadama Malunde-Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com