 |
Hapa ni katika ukumbi wa mikutano katika ofisi
ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga ambapo jana Aprili 22,2015 kumefanyika kikao maalum
mjini Shinyanga kilichoshirikisha
viongozi wa serikali wa mikoa na wilaya kutoka mkoa wa Simiyu na
Shinyanga kikilenga kukinusuru Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa
Shinyanga(SHIRECU) kutokana na changamoto
zilizopo za ushindani wa kibiashara kwenye zao la pamba ambalo ni tegemeo
kwa mikoa ya kanda ya ziwa.Kikao hicho kilihudhuriwa na wakuu wa mikoa ya
Shinyanga na Simiyu,wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa halmashauri za wilaya na
miji na watendaji mbalimbali wa serikali-picha zote na Kadama Malunde-Shinyanga |
 |
Mwenyekiti wa SHIRECU Robert Seleman Mayangela
akifungua kikao hicho ambapo alisema hicho ni kikao cha kazi na utekelezaji ili
kukabiliana na changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo. |
 |
Wajumbe wa kikao wakifuatilia kilichokuwa kinajiri ukumbini |
Mkuu wa mkoa wa
Shinyanga Ally Rufunga akitoa hotuba yake ambapo pamoja na mambo mengine aliitaka SHIRECU kuviendeleza vyama vya ushirika
ambavyo vinasuasua ,huku akiwatahadharisha viongozi wa serikali na wanasiasa
kuwa hawaruhusiwi kuwa viongozi ndani ya vyama vya ushirika ili kuepusha
migongano ya kimaslahi.
Wakuu wa wilaya wakiwa ukumbini
Meneja mkuu wa SHIRECU mkoa wa Shinyanga Joseph
Mihangwa akitoa taarifa ya shughuli za SHIRECU 1984 Limited ambapo alisema hadi
kufikia Mwezi Machi 2015 ina vyama vya Ushirika vya Msingi wanachama hai 500 na
vyama sinzia ( ambavyo havina kazi) 250
 |
Meneja mkuu wa
Shirecu mkoa wa Shinyanga Joseph Mihangwa alisema hadi kufikia Desemba mwaka 2014
walikuwa na rasilimali zisizoondosheka zenye thamani ya shilingi 47 bilioni
ambazo zinapaswa kuendelezwa na kuboreshwa vikiwemo viwanda vya kuchambua
pamba na kusindika mafuta.
|
Mihangwa alisema katika msimu
huu wa 2015/2016 wamejipanga kununua kilo milioni 15 za pamba katika mkoa wa
Shinyanga,Simiyu na Geita kwani uwezo wa pesa upo.
 |
Meza kuuu wakifuatilia kilichokuwa kinajiri ukumbini |
 |
Kikao kinaendelea |
Kikao kinaendelea ambapo wajumbe wa kikao hicho waliitaka Shirecu kuangalia uwezekano wa kuanza
kuongeza thamani kwenye zao la pamba ili kupata faida zaidi na kuachana na
mfumo wa kizamani wa kuuza pamba tu-picha zote na Kadama Malunde-Shinyanga
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com
Social Plugin