KITUO CHA RADIO ALNOOR CHATEKETEA KWA MOTO HUKO ZANZIBAR,MTANGAZAJI AJIRUSHA KUTOKA GOROFANI KUEPUKA MOTO HUO

KITUO cha kurusha matangazo ya radio cha dini ya Kiislamu cha Alnoor kimeteketea kwa moto ikiwemo studio zake tatu. Mkurugenzi mkuu wa Radio Alnoor, Mohamed Suleiman Tall, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo alisema chanzo chake kikubwa ni hitilafu ya moto katika kituo kikuu cha umeme.
 
Alisema moto huo ulianzia katika studio nambari tatu ambayo imeteketea huku vifaa vyote ikiwemo kompyuta pamoja na vifaa vingine muhimu vya mawasiliano ya redio  vimeteketea.
 
"Radio Alnoor imeteketea kwa moto ambapo studio zake tatu zimeharibika na tunakisia tumepata hasara Sh milion 82," alisema.

 
Tall alisema juhudi za kiufundi za kurudisha matangazo ya Radio Alnoor hewani kwa wasikilizaji wake zinaendelea hadi sasa.
 
"Tunafanya kila juhudi kuona kwamba wananchi wanapata matangazo ya Radio Alnoor, licha ya kujitokeza kwa hitilafu kubwa ya studio zake kuteketea kwa moto," alisema.
 
Kwa mujibu wa maelezo ya mtangazaji mmoja Rashid Salum, alisema tukio hilo limetokea majira ya saa nane za usiku huku chanzo kikubwa ni hitilafu za umeme.
 
Mmoja ya watangazaji wake Abubakar Fakih, amejeruhiwa kwa kuumia mguu baada ya kuruka kutoka ghorofa ya pili kwa ajili ya kujihami na moto huo.

 
"Moto ulikuwa mkubwa kiasi nililazimika kujirusha kutoka ghorofa ya pili hadi chini kwa ajili ya kujiokoa," alisema Fakih.
Radio Noor ni maarufu visiwani hapa ambayo hurusha matangazo yake zaidi yenye muelekeo na kutoa Elimu ya dini ya Kiislamu
via>>eddy blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post