Ukatili!! KICHANGA CHA MIEZI 6 CHATUPWA KICHAKANI HUKO KAHAMA

Maiti ya mtoto huyo

Mtoto wa kiume anayekadiriwa kuwa na miezi 6 ambaye hajatambulika jina lake wala makazi amekutwa amefariki dunia kichakani baada ya kutupwa na mtu asiyefahamika katika kijiji cha Mhongolo wilayani Kahama
Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Ally Manyama amesema kuwa  baada ya kufika eneo la tukio alikuta mwili wa mtoto huyo ukiwa umeviringishwa katika kitenge na kutupwa kichakani katika eneo hilo.
Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limethibitisha kutokea kwa tukio hilo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post