Wafanyakazi walioajiriwa na shirika la Reli Tanzania (TRL) wakitoa
mchanga kwenye kichwa cha treni ya mizigo kilichopata ajali usiku wa
kuamkia katika stesheni ya Gulwe, Wilaya ya Mpwampwa. Katika ajali hiyo
watu wawili wamefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa na kulazwa
katika hospital ya Benjamin Mkapa Wilayani Mpwampwa.
Sehemu ya mabehewa ya mafuta na ngano ambayo hayakusombwa na maji
katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika stesheni ya Gulwe,
hiyo imetokea saa 9.15 usiku. Treni hiyo ya Mizigo ilikuwa ikitokea Dar
es Salaam na kuelekea Mkoani Kigoma na ilikuwa na mabehewa yaliyobeba
ngano, sukari na mafuta.
Njia ya Reli iliyoondolewa na maji katika stesheni ya Gulwe Wilaya
ya Mpwampwa kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha maeneno
mbambali nchini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka akitoka
kwenye maji baada ya kuangalia kichwa cha treni kilichopata ajali na
kusombwa na maji katika stesheni ya Gulwe, Wilaya ya Mpwampwa, usiku wa
kuamkia leo, kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali
za nchi. Ajali hiyo imesababisha kifo cha watu wawili na wengine saba
kujeruhiwa na kulazwa katika hospital ya Benjamin Mkapa iliyoko wilayani
Mpwampwa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk, Shaaban Mwinjaka akimfariji
mmoja wa Majeruhi wa Ajali ya treni ya mizigo iliyotokea katika
Stesheni ya Gulwe Bw. Michael Lupatu wakati alipomtembelea katika
hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo Wilayani Mpwampwa leo mchana. Ajali
hiyo ya treni ya mizigo imetokea usiku wa kuamkia leo na kusababisha
kifo cha watu wawili na wengine saba kujeruhiwa.
(Picha na kitengo cha Mawasiliano Serikalini uchukuzi)
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553