Mfano wa Kuigwa !! KAMPUNI YA EASY FLEX PRODUCTION YA MJIN SHINYANGA YAANDAA HAFLA KUSAIDIA KAMBI YA WAZEE KOLANDOTO NA KITUO CHA WATOTO WENYE ULEMAVU CHA BUHANGIJA KATIKA MANISPAA YA SHINYANGA

Kulia ni  bi Happiness  Mwaja Kihama (Mkurugenzi wa Easy  Flex production )ambaye ni
mratibu wa mradi wa kuwasaidia wazee  kuchangia kambi ya  Kolandoto na Buhangija kutoka kampuni ya Easy Flex  Production ya mjini Shinyanga inayojihusisha na shughuli za uzalishaji wa kazi za wasanii katika mfumo wa Sauti na Video wakati akizungumza wakati wa mkutano wao na waandishi wa habari leo mjini Shinyanga katika ukumbi wa Karena Hotel,ambapo amesema kampuni yake kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa pamoja na wadau mbalimbali wameandaa hafla ya chakula cha wahisani.Amesema hafla hiyo inalengo la kuiamsha jamii na kukusanya fedha pamoja na mali kwa lengo la kuwasaidia jamii ya wazee waishio kwenye kambi ya Kolandoto pamoja na watoto wa shule ya maalum ya walemavu wa ngozi,wasioona,wasiosikia ya Buhangija mjini Shinyanga,ambapo halfa hiyo itafanyika tarehe 29 mwezi huu, katika ukumbi wa Karena hoteli kuanzia saa nane mchana,ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga.
Wa kwanza kulia ni
mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya hafla hiyo Sospeter Wilson Ntoke ambaye ameitaka jamii kujitokeza kusaidia watu wasiojiweza na kuacha dhana potofu ya kutegemea watu kutoka nje ya nchi  kwamba wao ndiyo wanapaswa kutoa misaada.Hivi karibuni kampuni ya Easy Flex production ilitembelea
kambi ya wazee ya Kolandoto pamoja na kituo  cha walemavu wa ngozi Albino kilichopo Buhangija mjini Shinyanga na kujionea changamoto mbalimbali zilizopo katika vituo hivyo na kukumbana na changamoto ya wazee( wanamme na wanawake) kutumia choo kimoja katika kambi ya wazee ya Kolandoto.
Mbali na changamoto ya choo ,kambi  wazee ya Kolandoto inakabiliwa na ukosefu wa jiko,vyandarua, pamoja na vitanda ambapo wazee hao wanalalia vitanda vibovu vilivyochoka  vya  miaka ya 70 ambavyo si salama kwa afya zao.

Waandishi wa habari wakichukua mawili matatu kwenye mkutano huo.Pia
baada ya kampuni ya Easy Flex Production kutembelea kituo cha kulea watoto wenye ulemavu wa ngozi cha Buhangija jumuishi chenye watoto zaidi ya 250  walijionea hali  halisi  ya kituo hicho kinachokabiliwa na changamoto ya ukosefu wa chakula, uhaba wa mabweni mavazi, vifaa vya kufanyia usafi,vitanda ambapo kitanda kimoja cha futi 2 kinalaliwa na watoto wawili.
Waandishi wa habari wakiwa katika ukumbi wa mikutano katika hoteli ya Karena leo mjini Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post