Majanga tena Geita!!! MFUNGWA ABAKA MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI PORINI

NB-Picha haiendani na tukio katika habari hapa chini

Mfungwa wa gereza la Butundwe  wilayani Geita mkoani Geita mwenye namba 224/2013 Godfrey Selemani(19) amembaka mwanafunzi wa shule ya msingi Luhuha kata ya Nyakagomba na tarafa ya Butundwe baada ya kumkuta anachanja kuni porini.

Tukio hilo limetokea tarehe 26/2/2014 majira ya saa ya tisa ambapo mwanafunzi mwenye umri wa miaka 15 alipokuwa anachanja kuni na wenzake watano.

Inadaiwa kuwa  wakati wakiendelea kuchanja kuni alipita mtu mmoja akiwa amevaa sare za wafungwa na baada ya muda mfupi mtu huyo alirudi akiwa uchi wa mnyama na akiwa amejipaka masizi kifuani huku akikimbia kuelekea walikokuwa wakichanja kuni.

Kufuatia hali hiyo walianza kukimbia kila mtu uelekeo wake huku wakipiga kelele za kuomba msaada lakini kwa bahati mbaya mwanafunzi huyo alijikwaa na kuanguka chini na ndipo mtuhumiwa alipomvamia na kumbaka.

Imeelezwa kuwa wakati mtuhumiwa akifanya kitendo hicho mwanafunzi aliyebakwa aliweza kumtambua kwa sura mbakaji.

Baada ya kufanya kitendo hicho mbakaji aliondoka  huku mwanafunzi huyo naye aliondoka kuelekea bahati nzuri alikutana  na mtu mmoja na kumsimulia majanga  yaliyomkuta  ndipo mtu huyo akampa msaada kwa kumpeleka kuripoti kituo cha polisi.

Akizungumzia tukio hilo mwanafunzi huyo(Jina tunalo) amesema kuwa siku hiyo aliondoka na rafiki zake  ambao hakuwataja majina yao kwenda porini kwa ajili ya kuchanja kuni na kumuona mfungwa huyo akaanza kuwakimbiza.

“Bahati mbaya niliteleza na kuanguka,baada ya kuanguka ndio akanikmata ana kunivulisha nguo na kunitendea unyama huo ambao umenisababishia maumivu makali,naiomba serikali kumchukulia hatua kali aliyenibaka”,alieleza mwanafunzi huyo.

Kwa upande wa mama mdogo anayeishi na binti huyo (Jina Tunalo)amesema kitendo alichofanyiwa binti yake ni cha  kinyama na yeye pia kuiomba serikali kumchukulia hatua kali mtuhumiwa huyo kwa unyama huo.

 Amongeza kuwa wamempeleka hospitali ya wilaya ya Geita na kupewa matibabu na kuambiwa warudi mwezi wa 5 ili apimwe tena kama amepata magonjwa ya zinaa kwani baada ya kupima hawakuona kama amepata maambukizi.

Mganga mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Geita Adam Sijaona amethibitisha kumpokea mwanafunzi huyo tar 27 na kumpatia matibabu hatimaye akamruhusu kwenda nyumbani

Kamanda wa polisi mkoani Geita kamishina msaidizi mwandamizi Leonard Paul amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo la mfungwa kubaka mwanafunzi na amesema kuwa mtuhumiwa ameshakamatwa na jeshi la polisi na taratibu za kumfikisha mahakamani zinaandaliwa ili akajibu tuhuma inayomkabili.

Inasemekana mfungwa huyo aliyebaka anatumikia kifungo cha miezi sita jela katika gereza hilo la Butundwe.
 Na Valence Robert-Geita

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post