IKULU YASEMA HAINA MUDA WA KUJIBU POROJO ZA ASKOFU KAKOBE


Kurugenzi  ya  mawasiliano  Ikulu  imesema  haina  muda  wa  kujibu  porojo  zilizotolewa  na  Askofu  wa  kanisa  la  Full  Gospel  Fellowship, Zachary  Kakobe  kwani  ina  kazi  kubwa  ya  kuwatumikia  watanzania....

Imesisitiza  kuwa  ofisi  ya  Kurugenzi  ya  mawasiliano  Ikulu  haifanyi  kazi  za  porojo  kama  sehemu  ya  kuendesha  utawala  wake, badala  yake  iko  makini  kutatua  matatizo  yanayowakabili  wananchi  kwa  kulinda  na  kuheshimu  demokrasia  na  kufuata  katiba  ya  nchi....

Kauli  hiyo  inatokana  na  waraka  maalumu  unaodaiwa  kutolewa  na  Askofu  Kakobe  na  kisha  kupelekwa  Ikulu.Hata  hivyo, kurugenzi  ya  mawasiliano  Ikulu  imesema  haijathibitisha  rasmi  kama  waraka  huo  umefika  katika  ofisi  hiyo.....

Akizungumza  juzi  na  gazeti  la  Jambo  Leo  kwa  njia  ya  simu,Mkurugenzi  wa  idara  ya  mawasiliano  Ikulu, Salvatory  Rweyemamu  alisema  serikali  si  lazima  ijibu  Porojo  zilizotolewa  na  Kakobe, kwani  Ikulu  ni  sehemu  nyeti  ya  kutumikia  wananchi  katika  maswala  ya  msingi  na  yenye  tija  kwa  taifa.....
"Yaani  unataka  niseme  mambo  ya  porojo  badala  ya  kuelekeza  majibu  yenye  kutatua  matatizo  ya  wananchi",
alisema na  kuongeza  kuwa  swala  hilo  lilishajibiwa  na  kaimu  katibu  mkuu  ofisi  ya  waziri  mkuu, Dr  Florence  Turuku  ambapo  alilitolea  ufafanuzi  wa  kutosha.

Waraka  huo  uliotolewa  kwenye  vyombo  vya  habari  na  Askofu  Kakobe  ulikuwa  ukieleza  namna  Ikulu  "ilivyotupa  kapuni"  majina  yote  ya  wapentekoste  waliopendekezwa  kuwa  wajumbe  wa  bunge  maalumu  la  katiba, hivyo  kuwafanya  wapentekoste  takribani  milioni  10  kukosa  mwakilishi  hata  mmoja...

Pia  waraka  huo  ulidai  kuwa  baada  ya  kukosa  uwakilishi, Ikulu  ilitoa  kauli  za  kejeli  kuwa, haijawahi  kupokea  jina  hata  moja  la  mpentekoste.
"Ofisi  yako  imeona  kwamba  ni  haki  hata  kwa  waganga  wa  kienyeji  kuwakilishwa  katika  bunge  hilo  kuliko  wapentekoste  kupata  mjumbe  hata  mmoja", ilisema  sehemu  ya  waraka  huo.

Hata  hivyo  baadhi  ya  wananchi  waliohojiwa  na  gazeti  la  Jambo  Leo  walisema  Askofu  Kakobe  amezoea  kulumbana  na  Serikali, hivyo  uamuzi  wake  hauna  mashiko.
"Tunajua  ana waumini  wengi  wanaomsikiliza, lakini  kwa  maswala  ya  kiserikali  ambayo  inaaminika  haina  dini  ni  vigumu  kuitabiria  mabaya, kwani  yeye  kama  mchungaji  alistahili  kukaa  pamoja  na  ofisi  husika  na  si  kwenda  kunukuu  vitabu  vitakatifu  kwa  kuitabiria  mabaya  serikali", Alisema  Patrick  Haule  ambaye  ni  Mwinjilisti.

Chanzo: Gazeti  la  Jambo  leo, tarehe  13  march 2014

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post