Makubwaaaa!!! MAJINA YA WANAFUNZI YAGEUZWA DILI GEITA,WAPEWA YA BANDIA KWA LAZIMA,MKUU WA SHULE,AFISA ELIMU MATATANI

Diwani wa kata ya Nyugwa katika wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita Charles Kabosoro akiongea na wanafunzi wa Shule ya sekondari Nyugwa wakiwemo wanafunzi waliopewa majina ya bandia ya kufanyia mtihani wa kidato cha pili mwaka jana ambao walimwita ili kujua hatma ya kutopewa majina yasiyokuwa yao

Katika hali isiyokuwa ya kawaida wanafunzi wa shule ya Sekondari Nyugwa iliyoko katika kijiji cha Mimbili kata ya Nyugwa wilaya ya Nyangw'hare mkoani Geita wameiomba serikali ya mkoa kuwachukulia hatua afisa elimu wa sekondari wa wilaya Bi Mosha pamoja na mkuu shule hiyo Lucas Joshua kwa kuuza majina yao na kuwalazimisha kuwapa majina yasiyokuwa yao wakati wana majina yao tena kwa kuyanunua kwa pesa.

Wakiongea kwa nyakati tofauti jana ,wanafunzi hao wamesema  mkuu wa shule hiyo Lucas Joshua  amekuwa ni kinara wa kuuza majina yao na kuwapa majina yasiyokuwa ya kwao na kuwataka kama wanataka ya kwao yaliyopotea kutakiwa kuyanunua kuanzia kiasi cha shilingi elfu 25  hadi elfu 30 kwa madai kuwa majina yao ya awali yanafuatwa mkoani kwa pesa.

Wanafunzi hao wamesema mwalimu huyo pamoja na kuuza majina yao amekuwa na tabia mbaya sana katika shule hiyo kwa kufuja mali za shule bila kufuata utaratibu.

“Kwa kweli hatupendi tabia za mwalimu mkuu,mbaya zaidi amekuwa akisema hakuna mtu yeyote wa kumgusa hata awe nani na yeye ndiyo mkuu na mwanafunzi ambaye hataki kutumia jina lililopo aache “, walisema wanafunzi hao.

Kwa upande wake mkuu huyo wa shule alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo alisema  yeye si msemaji na msemaji ni afisa elimu wa wilaya lakini pamoja matukia hayo cha kushangaza wanafunzi 11 waliofanya mtihani wa kuingia kidato cha tatu mwaka jana walifanya mtihani wao kwa kulazimishwa kutumia picha  na majina yasiyo ya kwao na Afisa elimu wa wilaya hiyo Bi Mosho.

Akizungumzia kuhusu tuhumu hizo afisa elimu wa sekondari wa wilaya Bi Mosha alikiri kulifahamu suala hilo  na kuhusu kuwafanyisha mtihani wanafunzi kwa majina yasiyokuwa ya kwao alidai kuwa  aliamua kufanya hivyo hili asivuruge mtihani uliokuwa ukiendelea na kuahidi kulishugulikia suala hilo kwa kumchukulia hatua kali mwalim huyo.

Naye Diwani wa kata ya Nyugwa katika wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita Charles Kabosoro akiongea na wanafunzi wa Shule ya sekondari Nyugwa wakiwemo wanafunzi waliopewa majina ya bandia ya kufanyia mtihani wa kidato cha pili mwaka jana ambao walimwita pamoja na wazazi ili kujua hatma ya kutopewa majina yasiyokuwa yao,amelaani kitendo hicho cha mwalim huyo pamoja na afisa elimu wa wilaya kuhujumu majina ya watoto wao na kuwalazimsha kuwapa ya majina ya bandia na kuiomba serikali kuwachukulia hatua kali wote waliohusika bila kujali mtu yeyote.

''Mimi kama diwani kata hii naona hata afisa eliu  anahusika kwani angekuwa hahusiki asingewambiwa wanafunzi wafanye mtihani kwa majina bandia kwa kulazimishwa na yeye na kuahidi kulichukulia hatua na mpaka sasa hajachukua hatua naye anahusika”,alisema diwani huyo.

Kitendo hicho cha kuuzwa kwa majina ya watoto kuuzwa na kupewa majina ya bandia kimewashangaza wakazi wa mkoa wa Geita pamoja na vitongoji vyake huku wanafunzi waliopewa majina bandia wakiwa hawajui pa kwenda.

Na Valence Robert-Geita



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post