Eneo la tukio |
Habari kutoka Manyoni mkoani Singida zinasema kuwa Basi la Bunda Express lililokuwa linatoka Dodoma kuelekea Mwanza limegonga Treni iliyokuwa inatoka Aghondi Itigi katika eneo la njia panda ya Itigi Na Singida.
Majeruhi 38 tayari wamepelekwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Manyoni.
Chanzo cha ajali inasemekana kuwa ni uzembe wa dereva ambapo inadaiwa dereva wa gari hakusimama wakati anajua anapaswa kusimama katika eneo hilo la njia ya treni.
Post a Comment