Mauaji Singida!! WANANCHI WAUA ASKARI WA WANYAMAPORI KWA KUMCHARANGA MAPANGA KISHA KUMCHOMA MISHALE NA PINDE,WAJERUHI PIA WATU WENGINE 17

Kamanda wa polisi mkoa wa SingidaGeofrey Kamwela  
Askari mmoja mhudumu wa wanyamapori  mkoani Singida ameuawa  na  watu wengine 17 kujeruhiwa vibaya baada ya kuchomwa mishale, pinde na kukatwa  mapanga na wananchi wenye  hasira kali.

Askari huyo  Athumani  Jumanne (40)  na watu wengine waliojeruhiwa wote wakazi wa Nduamughanga  Wilaya ya Singida, wanadaiwa kuvamiwa na wananchi zaidi ya 300 kutoka kijiji jirani cha Handa-Chemba  mkoani Dodoma wakitaka wapewe mifugo yao zaidi ya 150 iliyokamatwa kwenye hifadhi ya msitu.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Singida, Kamishina Msaidizi Mwandamizi Geofrey Kamwela  amesema  tukio hilo limetokea jana majira ya saa 7: 30 mchana, muda mfupi baada ya askari huyo na wenzake kukamata mifugo hiyo iliyokuwa inachunga kwenye  hifadhi ya msitu wa  asili wa Mgori.

Amesema wakiwa katika mapumziko, kundi la wananchi waliohamishwa kutoka kwenye hifadhi hiyo miezi miwili iliyopita, waliwavamia wakiwa na silaha mbalimbali za jadi na kuanza kuwashambulia.

Amesema askari huyo alikufa papo hapo, wakati wananchi 16 waliojeruhiwa wametibiwa   Zahanati na kuruhusiwa, isipokuwa mmoja ambaye amelazwa  katika hospitali ya mkoa  kwa matibabu.

Kamanda Kamwela  amesema  mbali na  kuua na kujeruhiwa, wananchi hao  wamepora  ng’ombe  wengine 68,  mbuzi 101, kondoo sita na punda watatu  na kutoweka nao kama njia  ya kulipiza kisasi.

Watu wawili wanashiliwa na jeshi la polisi na wengine wanaendelea kutafutwa kuhusiana na tukio hilo.

Credit-Chami wa matukio blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post