![]() | |
NB-siyo kanisa na mchungaji Polite Mabesa Na Valence Robert-Geita |
Mchungaji wa Kanisa la Emma wa Ngusu lililopo mtaa wa 14
Kambarage mjini Geita bwana Polite
Mabesa amejikuta katika kashfa ya kutorosha watoto wa kike na kuishi nao nyumbani kwake.bila idhini ya
wazazi wao kwa madai kuwa anawapatia huduma ya kiroho.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti
na waandishi wa habari wazazi wa watoto hao wamedai kuwa wanamshangaa
mchungaji huyo ambaye bado hajaoa kuishi
na mabinti wao bila ya wao kujua kwa madai anawapa huduma ya kiroho.
Akizungumzia suala hilo balozi wa mtaa wa 14 Kambarage Sospeter Makoko amesem aofisi yake tayari imepata taarifa za mchungaji kuishi na mabinti na kwamba anashangaa vyombo vya sheria kwanini vimekuwa bubu wakati taarifa hizo wanazo.
Aliongeza kuwa mbali na suala hilo Mchungaji huyo amekuwa kero mtaani kwao maana usiku wa manane amekuwa akipiga miziki jambo ambalo linahatarisha usalama katika mtaa huo kutokana na kelele.
Kufuatia hali hiyo waandishi wa habari walifanikiwa kufika
nyumbani kwa mchungaji huyo ili kupata ukweli,ambapo waliwakuta wasichana zaidi
ya saba ambao walikuwa wakiendelea na kazi za nyumbani kwa mchungaji huyo.
Aidha waandishi hao walifaikiwa
kumkuta mchungaji huyo na baada ya kutaka kujua ukweli mchungaji huyo alidai waandishi
wamemshtukiza ilifaa wampe taarifa mapema huku akiwaomba warudi siku nyingine
ofisini ili alitolee ufafanuzi suala hilo.
Post a Comment