MWALIMU AKAMATWA AKIWAFANYIA WANAFUNZI MTIHANI WA DARASA LA SABA IRINGA


NB.PICHA HAIHUSIANI NA TUKIO
Jeshi la  polisi  mkoani Iringa  linamshikilia mwalimu wa  shule ya msingi Makungu wilaya ya  Mufindi Bw Edwin Ambukile kwa  tuhuma  za  kuwasaidia majibu wanafunzi wa  darasa la  saba katika mtihani  wa Taifa  wa kuhitimu elimu ya msingi.
Kamanda  wa polisi mkoa  wa Iringa Bw Ramadhan Mungi amesema  kuwa tukio  hilo limetokea  Septemba 15 mwaka  huu  .
Alisema kuwa mwalimu  huyo ambae ni mwalimu wa masomo ya Sayansi katika  shule  hiyo pia alikuwa ni mwalimu wa masomo ya ziada ( katika  shule  hiyo na  sababu ya  kuwasaidia  wanafunzi majibu ni kutaka  kupata umaarufu kwa wanafunzi  watano aliokuwa akiwafundisha masomo ya  ziada aliopata  kuwaahidi kuwa watafaulu mtihani  huo.
Alisema  kuwa  mwalimu  huyo tarehe 11 septemba  alipokea mitihani kutoka kwa msimamizi  na baada ya hapo akafungua bahasha   ya masomo ya  Sayansi na kuanza  kufanya mwenyewe  na majibu kuyatuma kwa Sms kwa  mke  wake .
Hata  hivyo  siku ya mtihani mmoja kati ya wanafunzi  waliopata majibu hayo alipoingia katika  chumba  cha mtihani alionekana akitetemeka  kupita  kiasi na  hivyo msimamizi wa mitihani alipompekua alimkuta na majibu hayo na kueleza jinsi alivyosaidiwa na mwalimu  huyo .
Kamanda  wa  polisi alisema  siku ya mtihani  mwalimu Ambukile  alipangiwa kusimamia  shule  ya msingi Igomaa na  sasa amekamatwa na atafikishwa mahakamani  wakati  wowote kuanzia sasa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527