PETROLI YAUA WATATU KAHAMA

                     
WATU  watatu wamefariki  duniA baada ya dumu la petroli lililokuwa ndani ya nyumba walimokuwa kulipuka na kuteketeza nyumba katika kijiji cha  Nyangalata - Machimboni katika  kata ya  Lunguya  wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga ACP  Evarist Mangalla amesema tukio hilo  limetokea jana majira ya saa nne asubuhi na  kuwataja waliopoteza maisha kuwa ni  Maria Peter  (1), Hamis Masanja  (1) na Saida  Cosmas  (20).
Amesema vifo hivyo vilitokea wakati marehemu  Saida Cosmas  alipokuwa akiwasha  jiko  kwa ajili ya kupika  chakula  cha mchana ndipo aliingia shemeji yake aliyefahamika kwa jina la  Kulwa Bundala  na kuanza kimimina Petroli  kutoka dumu moja kwenda jingine.
Kamanda Mangalla amefafanua kuwa  mara baada ya Kulwa Bundala kuanza  kumimina petroli kwa kuhamishia ndani ya dumu jingine huku Saida Cosmas   akiendelea na pilikapilika za kuwasha moto  ndipo moto mkubwa ulitokea ghafla na kulipuka na kusababisha vifo  vya watu watatu.
Hata hivyo baada ya kutokea kwa mlipuko wa moto Kulwa Bundala alifanikiwa kutoroka  na hivi sasa  jeshi la polisi linaendelea kumtafuta.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments