Na WMA - DODOMA.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Chande, amefurahishwa na uelewa mkubwa ulioonyeshwa na wanafunzi waliopata elimu ya vipimo katika banda la Wakala wa Vipimo - (WMA), kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane.
Akizungumza leo Agosti 6, 2026 baada ya kuzungumza na wanafunzi hao aliowakuta katika Banda la WMA, Viwanja vya Dkt. John Malecela Nzuguni, Dodoma, Naibu Waziri ambaye pia alikuwa katika ziara ya kutembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho, alisema ni hatua nzuri kwa WMA kuanza kuwafundisha watoto umuhimu wa vipimo sahihi wakiwa wadogo.
“Nimefurahishwa sana. Watoto hawa wameelewa kuwa kipimo sahihi ni haki ya kila mtu. Hawa ndio Maafisa Vipimo wa kesho,” alisema.
Awali, Naibu Waziri Chande alipowakuta wanafunzi hao bandani aliwauliza maswali mbalimbali kuhusu vipimo na waliweza kujibu kwa ufasaha.
Wanafunzi hao wa Shule ya Msingi Blessed Mabuba iliyopo jijini Dodoma, ambao waliongozana na mwalimu wao Irene Ketta, ambaye pia alipongeza WMA kwa kujielekeza katika utoaji elimu ya vipimo mashuleni hatua ambayo alisema imewawesha wanafunzi kueleza tofauti ya kipimo sahihi na kisicho sahihi, umuhimu wa kusoma lebo na jinsi ya kutumia mizani.
“Niwape pongezi WMA. Kama tutaendelea kuwapa elimu hii watoto wetu, tunajenga Taifa la wafanyabiashara waaminifu na walaji wenye ufahamu. Huu ndio msingi wa uchumi imara,” alisema Mwalimu Ketta.
WMA imeahidi kuhakikisha elimu ya vipimo inaenea kwa jamii nzima kupitia utoaji elimu kwa makundi mbalimbali wakiwemo wanafunzi.
[12:15 PM, 8/6/2026] Okuly Blog: WMA YAWAFUNDISHA WATOTO VIPIMO: NAIBU WAZIRI MALIASILI APONGEZA [8:14 PM, 8/6/2026] Okuly Blog: 
Na WMA - DODOMA.
Wajasiriamali wa kikundi cha Hapa Kazi kutoka Shehia ya Mtemani Wingwi, Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba wametembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane yanayofanyika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela, Nzuguni, jijini Dodoma.
Katika ziara hiyo iliyofanyika leo Agosti 6, 2026, wajasiriamali hao wameshukuru kupata elimu kuhusu matumizi sahihi ya vipimo, ufungashaji bora wa bidhaa na mbinu za kuongeza ushindani wa bidhaa zao sokoni.
Mwakilishi wa kikundi hicho, Asha Mwiaka Haji, amesema maonesho hayo yameendelea kuwafungua macho na kuwaongezea uelewa mkubwa kuhusu vigezo vinavyopaswa kuzingatiwa katika biashara ili bidhaa zao ziweze kupenya kwenye masoko.
“Tumefurahi sana kufika banda la WMA maana sisi pia tuna Wakala kama hii Zanzibar. Tumejifunza jinsi ya kutumia mizani, kuweka lebo sahihi na umuhimu wa vipimo katika biashara yetu, elimu ambayo pia tumekuwa tukiipata kupitia Wakala yetu ya Vipimo Zanzibar,” alisema.
Asha ameeleza kuwa kikundi chao kinajishughulisha na usindikaji na uuzaji wa bidhaa mbalimbali zikiwemo mwani, mafuta ya mgando, sabuni za mwani pamoja na dawa za asili.
Aidha, amesema ushiriki wao katika maonesho hayo umewaongezea ujuzi na uelewa zaidi kuhusu matumizi sahihi ya vipimo, mfumo wa alama za mistari (barcodes) na mbinu bora za kufungasha bidhaa.
“Tunawashukuru WMA kwa elimu hii. Tukirudi kwetu, tutaendelea kuwaelimisha pia wajasiriamali wengine ili tuweze kuzalisha bidhaa zenye ubora na zinazokidhi viwango vya soko,” alisema Asha.
Aidha, Asha amewahimiza wajasiriamali wenzake kushirikiana kwa karibu na maafisa wa Serikali katika ngazi ya shehia na wilaya ili kubuni mikakati itakayoongeza thamani ya bidhaa zao na kuchochea ukuaji wa uchumi.
Wakala wa Vipimo (WMA) inafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na Wakala wa Vipimo Zanzibar (ZAWEMA)







Social Plugin