
Kwa miaka minne ya ndoa yangu, nilikuwa kama mgeni ndani ya nyumba yangu mwenyewe. Mume wangu alikuwa tajiri wa kutupwa anaendesha biashara kadhaa jijini Mwanza, anamiliki magari ya kifahari na hata nyumba kadhaa.
Lakini pamoja na utajiri wake wote, hajawahi kunipa hata shilingi mia moja kwa hiari. Kila mara nilipohitaji hela ya matumizi au hela ya kwenda saluni, ilikuwa lazima niombe kwa unyenyekevu hadi nahisi kama ombaomba. Hata nguo zangu nyingi zilinunuliwa na dada zangu au marafiki walionionea huruma.
Social Plugin