Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UDIWANI ARUSHA MJINI DOGO JANJA YUMO


Na Woinde Shizza,Arusha

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha kimetangaza rasmi majina ya wagombea wake wa nafasi za udiwani kwa Jimbo la Arusha Mjini, kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Oktoba mwaka huu, huku jina la msanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya, Abdulazizi Chende ‘Dogo Janja’ likivuta hisia za wengi.

Akitangaza majina hayo leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za CCM Mkoa wa Arusha,  Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM, Saipurani Ramsey alisema uteuzi huo umezingatia vigezo mbalimbali vikiwemo historia ya uaminifu kwa chama, ushiriki hai katika shughuli za kijamii, ushindi kwenye kura za maoni, pamoja na uwezo wa kushirikiana na wananchi na viongozi.

“Tumefanya mchujo wa kina kuhakikisha tunapata wagombea wenye maadili, uadilifu na uwezo wa kutekeleza majukumu ya udiwani kwa ufanisi,” amesema Ramsey.

Miongoni mwa majina yaliyotangazwa, Abdulazizi Chende (Dogo Janja) ameteuliwa kugombea nafasi ya udiwani katika Kata ya Ngarenaro, hatua inayotajwa kuleta upepo mpya katika medani ya siasa za Arusha Mjini.

Ramsey amewataka wagombea wote kutumia kampeni zao kuhamasisha mshikamano na maendeleo ya jamii, badala ya kugawa wananchi kwa misingi ya kisiasa.

Hii ndiyo Orodha ya Wagombea Wateule  wa Jimbo la  Arusha Mjini


Engutoto: Hamza Juma


Moivaro: Philemon Mollel


Levolosi: Abbas Mustafa


Themi: Melace Kinabo


Terat: Julias Sekeyani


Ngarenaro: Abdulazizi Chende (Dogo Janja)


Olorien: Zacharia Mollel


Kati: Abdulrasul Tojo


Osunyai: Elirehema Nnko


Kaloleni: Maximilian Iranghe


Sekei: Emanuel Kisira


Lemara: Matuyani Laizer


Unga-Limited: Mahamudu Omari


Sokoni One: Muksini Juma


Sombetini: Godfrey Kitomari


Sinoni: Peter Inyasi


Olmoti: Robert Komani


Moshono: Siriel Mbise


Eleray: Losioki Laizer


Kimandolu: Abrahamu Mollel


Muriet: Credo Kifukwe


Baraa: Jacob Mollel


Daraja Mbili: Prosper Msofe


Sakina: Hillar Mollel



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com