

Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Solwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Awadh Mbaraka Aboud, amefariki dunia Julai 19,2025 katika ajali iliyotokea eneo la Ibadakuli, barabara kuu ya kuelekea Shinyanga Mjini, baada ya bajaji aliyokuwa akisafiria kugongwa na basi la abiria la Kampuni ya Frester.
Taarifa zinaeleza kuwa marehemu alikuwa safarini kutoka eneo la Kolandoto kuelekea Shinyanga Mjini akiwa ndani ya bajaji, kabla ya kugongwa na basi la kampuni ya Frester, na kusababisha majeraha makubwa yaliyompelekea kufariki dunia pamoja na mtu mwingine.
Msiba huu mkubwa umeacha simanzi kwa familia, wananchi wa Kata ya Solwa, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na jamii nzima ya Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.
Kupitia mitandao ya kijamii, Mbunge wa Jimbo la Solwa, Mheshimiwa Ahmed Ally Salum, ameeleza masikitiko yake makubwa kufuatia msiba huo:
Mhe. Ahmed Salum ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wakazi wote wa Kata ya Solwa, akiwasihi kuwa na moyo wa subira na kuendelea kuenzi mema ya marehemu.
Malunde Media tunatoa pole kwa familia ya marehemu, wananchi wa Solwa, viongozi wenzake, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.
soma pia
Social Plugin