Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

NDUMBARO AREJEA ULINGONI:AAHIDI MAENDELEO ZAIDI SONGEA MJINI


Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Songea mjini Dkt. Damas Ndumbaro akikabidhiwa  fomu na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya James Mgego katika ofisi ya CCM wilaya manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma 

Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma 

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Dkt. Damas Ndumbaro, amechukua fomu ya kutetea kiti chake tena katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. 

Katika hatua hiyo Ndumbaro ameambatana na mkewe, Bi. Frola Mdima, ofisi ya  CCM wilaya, ambapo Katibu wa CCM wilaya, James Mgego, amemkabidhi fomu.

Ndumbaro amesisitiza kuwa kinachomchochea kurudi kwake ulingoni ni kuendeleza miradi ya maendeleo aliyoianzisha kipindi chake cha kwanza, ukiwemo ujenzi wa madarasa 244 yenye thamani ya shilingi bilioni 5.234 pamoja na madawati, meza na viti

Pia ameanzisha mashindano ya "Ndumbaro Cup" akiwa amewagawia vijana mipira 96 na jezi 96, ili kuwachochea kushiriki michezo, kukuza afya, nidhamu na vipaji  . 

Aidha, huduma za msaada wa kisheria zimeanzishwa chini ya kampeni ya Mwenge wa Uhuru kwa ajili ya kutoa ushauri bila malipo kuhusu ndoa, ardhi na urithi  .

Akiangazia mchango wake katika sekta ya afya,ambayo iligharimu kiasi cha shilingi bilioni 6.735 

pia Ndumbaro alijenga vituo vya afya vinne na zahanati  nne na Hospitali ya Rufaa moja

Ndumbaro pia alikabidhi vifaa tiba muhimu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma Desemba 2024, ikiwa ni sehemu ya jitihada zake za kupunguza muda wa wagonjwa hospitalini na kuboresha huduma za physiotherapy  . 

Alisimamia ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Songea, akisisitiza umuhimu wa ubora na ukamilifu wa mradi huo ili kuwapatia wananchi huduma bora kwa wakati  . 

Vivyo hivyo, kupitia juhudi zake za ubia na serikali, mradi wa maji ulioteuliwa na Rais Samia Suluhu uliwezesha mradi wa maji kukamilika mjini Songea, kwa gharama ya TZS bilioni 145.8, mradi ulioleta usambazaji wa maji safi kwa mamia ya kaya  .





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com