Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MWANASIASA MZALENDO AREJEA ULINGONI:MHAGAMA ACHUKUA FOMU KUENDELEZA HUDUMA KWA UMMA




Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Madaba Mheshimiwa Joseph Kizito Mhagama akiwa tayari ameshachukua fomu ya kutetea kiti chake cha ubunge katika jimbo la Madaba 

Na Regina Ndumbaro 

Madaba-Songea 

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Madaba, Mheshimiwa Joseph Kizito Mhagama, ameonyesha dhamira yake ya dhati ya kuendelea kulitumikia taifa kupitia jimbo hilo kwa kuchukua rasmi fomu ya kugombea tena ubunge.

Hatua hiyo imeashiria nia ya kuendeleza mafanikio ya maendeleo aliyoasisi katika awamu zilizopita, akiwa na lengo la kuinua ustawi wa wananchi wa Madaba kwa vitendo.

Mhagama ambaye amekuwa chachu ya maendeleo katika maeneo ya afya, elimu, barabara na umeme vijijini, amesisitiza kuwa dhamira yake bado ni thabiti katika kuhakikisha huduma bora kwa wananchi. 

Akiwa kiongozi mwenye rekodi ya uwajibikaji na uzalendo, amesema kuwa kazi kubwa iliyoanzishwa inahitaji kukamilishwa kwa kasi na weledi zaidi.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu, Mhagama amewashukuru wananchi kwa ushirikiano mkubwa waliompa katika kipindi cha nyuma, huku akiahidi kuendeleza uhusiano wa karibu uliopo kati yake na wananchi. 

Amesisitiza kuwa endapo atapewa ridhaa tena, atahakikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo unafanyika kwa uwazi, kasi na ufanisi katika kila kata ya jimbo hilo.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com