Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MKUU WA WILAYA YA BAGAMOYO AYAPONGEZA MAKANISA KUOMBEA AMANI YA NCHI

Diwani wa kata ya Bwilingu Nasser Karama akiagana na Mch. Joseph Hananja. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bw. Shaibu Ndemanga

NA. ELISANTE KINDULU, CHALINZE 

MKUU wa Wilaya ya Bagamoyo, Bw. Shaibu Ndemanga, ameyapongeza makanisa yanayounda Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kwa ajili kongamano la kuliombea  Taifa, leo katika viwanja vya polisi katika halmashauri ya Chalinze,Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani.

Kongamano hilo limeandaliwa na CCT kupitia matawi yake ya Chalinze na limehudhuriwa na waumini kutoka zaidi ya makanisa kumi yanayounda jumuiya hiyo.

Dhumuni  la kongamano hilo ni kuliombea Taifa la Tanzania na kuhimiza amani na mshikamano nchini.

" Ninawapongeza viongozi wa CCT  mkiongozwa na Mwenyekiti wenu, Mchungaji Joseph Chuma wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), kwa kuonyesha maono makubwa ya kiroho na uzalendo kwa taifa letu", amesema mkuu wa Wilaya.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya alisisitiza mshikamano kwa waumini na kuwataka wawe mabalozi wa amani bila kusahau malezi kwa vijana wetu dhidi ya madawa ya kulevya.

Kongamano hilo, lilihudhuriwa pia na  Mchungaji Richard Hananja, ambapo aliwahimiza waumini kuendelea kusimama katika nafasi yao ya maombezi kwa ajili ya Taifa huku akisisitiza kuwa kanisa lina jukumu kubwa la kuiongoza jamii kiroho na kijamii.

Kongamano hilo limehudhuriwa na waumini mbalimbali wa kiroho pamoja na viongozi wa Serikali kutoka mjini Chalinze na Wilaya ya Bagamoyo kwa ujumla.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com