Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

SULEIMAN NASSOR SAID ‘KING OIL’ ACHUKUA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA ITWANGI


Suleiman Nassor Said 'King Oil'
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga na mfanyabiashara wa mafuta, Suleiman Nassor Said maarufu kama King Oil, leo Juni 30, 2025, amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya chama chake kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo Jipya la Itwangi.

Jimbo la Itwangi ni jimbo jipya lililokatwa kutoka Jimbo la Solwa, mkoani Shinyanga.

Suleiman Nassor Said ambaye ni mzaliwa wa Tinde, amesema ameamua kuchukua fomu hiyo ili kuendeleza juhudi zake za kuwaletea wananchi maendeleo, akitumia uzoefu wake wa kuwasogezea huduma mbalimbali za kijamii.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com