Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

WAKILI PETTER MADELEKA AIVAA OFISI YA MSAJILI MSAIDIZI WA NYARAKA MKOA WA TANGA



Wakili Petter Madeleka

Na Hadija Bagasha Tanga

WAKILI Peter Madeleka ameiandikia barua ofisi ya msajili msaidizi wa nyaraka mkoa wa Tanga akimuomba kuondoa  pingamizi lililowekwa  kwenye kiwanja Plot namba 7 kilichopo Raskazone jijini Tanga  kutekeleza amri ya  mahakama.

Madeleka ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga mara baada ya kufika kwenye ofisi ya Msajili Msaidizi wa Nyaraka  mkoani Tanga kwa ajili ya kufanya upekuzi  na kujua hadhi ya kiwanja hicho.

Wakili huyo amesema pingamizi hilo liliwekwea mwaka 2014, na wakala wa Majengo Tanzania (TBA) zuio ambalo mahakama iliamuru kuondolewa baada ya kubaini kuwa halikuwa na sababu ya msingi ya kuwepo kwenye kiwanja hicho.


“Kwa mujibu wa sheria zuio lolote linalowekwa baada ya mwaka mmoja linakwisha muda wake,  lakini zuio hili licha ya mahakama kuamuru liondolewe  bado ofisi ya Msajili Msaidizi wa Nyaraka inaendea  kulitambua  na mteja wangu kwa sasa hawezi kufanya kitu chochote kwenye eneo hilo,”amesema Madeleka.

Madeleka amesema haada ya mteja wake kufika mahakama kuu kanda ya Tanga na baadae mahakama  ya rufani ya Tanzania na uamuzi kutoka wa kuondolewa kwa pingamizi hilo ,hatua itakofuata ni kupeleka jambo hilo kwa Muheshimiwa Rais ambaye kwa sasa ndiye anayeweza kutoa kauli juu ya  jambo hilo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com