CRDB YAKABIDHI MADAWATI KIBONDO, MWENDELEZO WA KAMPENI YA KETI JIFUNZE


Meneja wa CRDB Kanda ya Magharibi Ndg Jumanne Wambura Wagana amekabidhi madawati 40 kwa shule ya msingi Kasebuzi Mkoani Kigoma ambapo madawati hayo yamepokelewa na mkuu wa Wilaya ya Kibondo Mh. Aggrey John Magwaza ikiwa ni mwendelezo wa benki hiyo ya CRDB katika kutekeleza sera yake ya uwekezaji kwa jamii na  kampeni ya KETI JIFUNZE inayolenga kupunguza uhaba wa madawati mashuleni.

 Akipokea Madawati hayo Mkuu wa Wilaya ya Kibondo  Mh. Aggrey John Magwaza ameishukuru Benki ya  CRDB kwa msaada huo mkubwa na kuahidi kuendelea kuwapa ushirikiano mkubwa zaidi kibiashara huku akiwasisitiza wazazi walimu na wanafunzi kuendelea kutumia Huduma za CRDB na kuwaasa wadau wengine kuiga mfano huo na kurudisha kwa jamii.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post