DKT. YONAZI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA OXFORD POLICY MANAGEMENT

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi akizungumza na Wataalam kutoka Oxford Policy Management Ofisini kwake tarehe 09 Mei, 2024 Jijini Dodoma.

Na Mwandishi wetu- Dodoma

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amekutana na kufanya mazungumzo na Wataalam kutoka Oxford Policy Management kuhusu Uwezekano wa matumizi ya akili bandia (Artificial Intelligence and Machine Learning) katika kufanya mapitio ya matumizi ya umma (Public Expenditure Review).

Kikao hicho kimefanyika tarehe 09 Mei 2024 ofisini kwake Jijini Dodoma ambapo Dkt. Yonazi amesema pia lengo la kikao hicho ni kujadili kuhusu makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto (ECD) nchini Tanzania.

Ikumbukwe Serikali ya Tanzania ilizindua Programu ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali yam Mtoto (PJT-MMMAM) mwaka 2021 kama mpango mkuu wa kuzileta pamoja Wizara na wadau mbalimbali ili kuboresha Makuzi na maendeleo ya awali ya Watoto kuanzia kuzaliwa hadi umri wa miaka 8.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post