MSAJILI WA HAZINA AZUNGUMZA NA KAMPUNI YA UCHIMBAJI MADINI YA PERSEUS

 

DODOMA

Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, Aprili 20, 2024 amefanya mazungumzo na ujumbe kutoka Kampuni ya uchimbaji Madini ya Perseus ya nchini Australia iliyowakilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Jeff Quartermaine pamoja na Afisa Fedha Mkuu wa kampuni hiyo, Lee Anne de Bruin.

Kampuni ya PERSEUS imenunua hisa za Kampuni ya ORECORP iliyokua inamiliki mgodi wa Nyanzaga uliopo Geita.

Kikao hicho kilichofanyika jijini Dodoma, pamoja na mambo mengine, Perseus imekubali kuongeza asilimia 4 ya hisa za Serikali "Free Carried Interests" na kuifanya Serikali ya Tanzania kumiliki asilimia 20 ya mgodi huo kutoka asilimia 16 za awali.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post