MBUNGE MTATURU ACHANGIA MABORESHO YA MIUNDOMBINU YA ELIMU




JITIHADA za Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Mhe Miraji Mtaturu kwa kushirikiana na wanachi zimesaidia kukamilisha kazi ya upauaji wa madarasa mawili katika Shule Shikizi ya Mwitumi hatua itakayoondoa changamoto ya watoto kusafiri umbali wa kilomita 9 na kuvuka mito miwili kufuata shule mama ya Msingi Nkundi.

Katika jitihada hizo wananchi walitumia nguvu yao kujenga hadi usawa wa Lenta na mbunge akawaunga mkono kwa kutoa Sh Milioni 13 ambazo zilinunua Bati 110, mbao zote na Saruji ya kupiga lipu na Sakafu.

Akizungumza na kituo hiki April 24,2024,Mtaturu amesema kukosekana kwa madarasa hayo kumesababisha utoro wa wanafunzi wakati wa masika na hivyo kushusha kiwango cha ufaulu.

Amewashukuru wananchi wa Kitongoji cha Mwitumi, Kijiji cha Nkundi Kata ya Kikio kwa Ushirikiano mkubwa walioutoa wa kushirikiana nae na kumaliza shughuli ya ujenzi wa Darasa

"Hatimaye imewezekana kwa kushirikiana na wananchi tumepaua vyumba viwili vya madarasa katika kuhakikisha changamoto ya watoto wanaosafiri mwendo mrefu na kuvuka mito miwili kufuata shule mama ya Msingi Nkundi inaisha,nawashukuru sana wananchi kwa jitihada zenu,".ameshukuru.

#VitendoVinasautiKulikoManeno#SingidaMashariki#TunaendeleaKuwafikia#

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post