RC MACHA AFUNGUA RASMI SEMINA YA FAMILIA,MALEZI,BIASHARA NA HUDUMA ZA AFYA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO

 



Na Marco Maduhu,SHINYANGA
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha,amefungua Rasmi Semina ya Familia,Malezi,Biashara na huduma za Afya, ambayo inaendeshwa na Kanisa la Waadventista Wasabato Ukanda wa dhahabu Nyanza Gold Belt Field NGBF.

Semina hiyo imeanza kutolewa Aprili 2,2024 ambayo itakwenda hadi Aprili 27 mwaka huu Siku ya Jumamosi,imekutanisha watu mbalimbali ambayo inafanyika katika ukumbi wa Makindo.
Macha akizugumza wakati wa kufungua Semina hiyo, imelipongeza Kanisa la Waadventista Wasabato kwa kuendesha Semina hiyo ambayo inathamani kubwa kwa taifa, kwa kutoa masomo ya Familia na Makuzi,Afya pamoja na Biashara.

“Nalipongeza sana Kanisa la Waadventista Wasabato,ni Kanisa ambalo lenye Mahaghaiko makubwa katika kuhakikisha Makuzi ya Vijana yanakuwa kwenye Maadili mema, sababu sasa hivi hapa nchini kuna Janga la Mmomonyoko wa Maadili ya Vijana, na Taifa bora linajengwa na Malezi bora na Makuzi,”amesema Macha.
“Masomo haya ya Familia yanakumbusha wazazi kulea watoto wao katika Maadili Mema, na siyo kuwaacha wakijilea wenyewe na hatimaye kusababisha watoto kuwa na Maadili Mabovu,”ameongeza Macha.

Amesema kwa upande wa Masomo ya Afya, ameitaka jamii kuzingatia lishe bora, sababu Magonjwa mengine hasa yasiyo ya kuambukiza husababishwa na Mtindo Mbovu wa Maisha, na kwamba kupitia Mafunzo hayo yanaijenga jamii yenye Afya Bora.
Aidha, amesema kupitia Masomo ya Biashara,amewataka Wafanyabiashara wawe na hofu ya Mungu, na kufanya biashara zao kwa haki bila ya kuchakachua bidhaa, pamoja na kulipa Kodi ya Serikali.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa, ametoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa Amani, pamoja na Rais Samia na wasaidizi wake,ili awe na maono mazuri ya kuiongoza Nchi katika kweli na haki, sababu Nchi ikiwa na Amani itakuwa na Maendeleo.
Naye Askofu wa Jimbo la Ukanda wa dhahabu (NGBF) Kanisa la Waadventista Wasabato Enock Sando, amesema Kanisa hilo limeendelea kujipambanua katika ulimwengu kote na kugusa jamii, kuisaidia kujitegemea kupitia Semina za Biashara ili wawe na Fikra Chanya ya kujikwamua kiuchumi sababu Mungu hapendezwi na Umaskini.

Amesema Kanisa hilo pia lina amini katika Afya, sababu bila Afya hakuna Maendeleo, ndiyo maana katika Semina hiyo mafunzo ya Afya yanatolewa, pamoja na Masomo ya Kaya na Familia ili kuwe na Taifa lenye Umoja,Mshikamano na Mahusiano Mazuri.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI👇👇
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha akizungumza wakati akifungua Semina hiyo.
Askofu wa Jimbo la Ukanda wa dhahabu (NGBF) Kanisa la Waadventista Wasabato Enock Sando.
Awali Mchungaji Mstaafu Wilbert Nfumbusa akitoa Somo la Kaya na Familia.
Awali Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Shinyanga (TCCIA) Jonathani Manyama akitoa Somo la Biashara kwenye Semina hiyo.
Awali Afisa Muuguzi Sherida Madanka akitoa Somo la Lishe kwenye Semina hiyo.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Kwaya ya Lubaga Mara Nassa ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya SAC ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya Lubaga Mara Nassa ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya SAC ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kamati ya Maandalizi ya Semina hiyo ikiimba kwenye Semina.
Picha ya pamoja ikipigwa kwenye Semina hiyo.
Picha ya pamoja ikipigwa ikipigwa Semina hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post