
Miongoni mwa faida nyingi alizoeleza ni pamoja na kupata mazao yenye ubora, yasiyoharibiwa kirahisi na wadudu pamoja na kupata mavuno ndani ya muda mfupi.
Sambamba na faida hizo Edward pia ameeleza matarajio yake kwa Bajeti ya kilimo kwa Mwaka 2024/2025 kuwa ni kuendelea kupata mbegu hizo zinazozalishwa na taasisi zinazotambulika nchini pamoja na kupata pembejeo kwa urahisi zaidi ili kuendelea kupata mazao bora.
Kwa upande wake, Agnes Sachi ambaye pia ni kijana anayejihusisha na Kilimo cha Mbogamboga jijini Arusha ameeleza namna kulima kwa kutumia mbegu na miche bora kulivyomnufaisha na matarajio yake kuelekea bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2024/2025.
Social Plugin