BILIONI 161.4 ZA RAIS DKT SAMIA ZAIWEZESHA TANGA UWASA KUTEKELEZA MIRADI 20 YA KIMKAKATI

 

MKUU wa wilaya ya Muheza Zainabu Abdallah wa kwanza kushoto akikapata utepe kuashiria makabidhiano ya mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Maji Taka wilayani Muheza pamoja na kukabidhi Vyoo vilivyojengwa ikiwa ni sehemu ya Ujenzi wa Mradi huo kwa shule ya Sekondari Bonde,Shule ya Msingi Mdote na Soko la Majengo wilayani Muheza uliotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) Kulia Diwani wa Kata na anayefuatia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Rashid Shabani

MKUU wa wilaya ya Muheza Zainabu Abdallah akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo
Kaimu Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Rashid Shaban akizungumza kuhusu mradi huo

Mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari Bonde akieleza taarifa yake wakati wa makabidhiano hayo
Sehemu ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Bonde wakiwa kwenye halfa hiyo ya makabidhiano

Na Oscar Assenga, MUHEZA

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa ) wamesema katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt Samia Suluhu Serikali imewawezesha ujenzi wa miradi ya kimkakati 20 ya maji safi yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 161 ambayo imekuwa chachu kubwa kuwezesha wananchi kupata huduma ya maji safi na hivyo kuondokana na changamoto walizokuwa nazo awali.

Hayo yalisemwa leo na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) Mhandisi Rashid Shaban wakati wamekabidhi mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Maji Taka wilayani Muheza pamoja na kukabidhi Vyoo vilivyojengwa ikiwa ni sehemu ya Ujenzi wa Mradi huo kwa shule ya Sekondari Bonde,Shule ya Msingi Mdote na Soko la Majengo wilayani Muheza.

Mhandidi Shaban alisema pamoja na hilo pia ipo miradi 6 ya maji taka yenye thamani ya Bilioni 4.2 ukiwemo wa ujenzi wa miundombinu ya kupokea na kuchakata majitaka wenye thamani ya Bilioni 1 ambao umetekelezwa na hivyo kusaidia kuondosha kero ambayo ilikuwa ikiwkumba wananchi.

Alisema kutokana na uwezeshwaji huo kwa sasa mamlaka hiyo inatoa huduma ya maji safi na salama kwa wastani wa asilimia 92.5 ya wakazi wa Jiji la Tang (96.1%), Pangani (70%) na Muheza (71%) ambapo miaka mitatu iliyopita kabla ya utawala wa Serikali ya awamu ya sita huduma ya maji ilikuwa inapatikana kwa wastani wa asilimia 83.2 ya wakazi hao (Tanga 89%, Muheza 33% na Pangani 60%).

Aidha alisema hivi sasa maji safi yanapatikana kwa wastani wa saa 15 kwa siku katika miji ya Muheza ambapo miaka mitatu iliyopita huduma ya maji ilikuwa inapatikana kwa wastani wa masaa matatu na wakati mwengine siku moja baada ya Juma Zima.

Akizungumzia huduma ya uondoshaji wa maji Taka, Kaimu Mkurugenzi huyo alisema huduma hiyo hufanywa kupitia mtandao wa mabomba unaowahudumia wakazi wapatao 20,615 sawa na asilimia 5.2 ya wakazi Tanga Mjini, Maeneo ya Muheza, Pangani na maeneo ya pembezoni mwa Jiji la Tanga ambayo hufanywa kwa kutumia mifumo mingine ya uondoshaji majitaka ikiwemo vyoo vya shimo na vyoo vya kunyonywa na magari vikishajaa.

Hata hivyo akielezea ujenzi wa vyoo na ombi la kukabidhi kwa watumiaji ,Mhandisi Rashid alisema kwamba kwa kua mradi huo unahusiana na usafi wa mazingira,Tanga Uwasa iliona ijenge aina hiyo ya vyoo ili kuonesha mfano wa vyoo bora vinavyotakiwa kujengwa katika jamii ikiwemo faida ambazo zinapatikana kupitia mradi huo.

Alisema faida ni kuwaepusha uchafuzi wa maji ya ardhini, uwepo wa huduma karibu na wananchi kupitia gari la kunyonya majitaka toka na hivyo kuondoa changamoto ya utupaji mbali na wakati mwengine katika maeneo yasiyorasmi.

“Pia kupungumza changamoto ya ufinyu wa vyoo katika shule za Msingi Mdot,Shule ya Sekondari Bonde na Soko la Majengo ambapo gharamaa nafuu kwani kutumia eneo dogo la ardhi na hudumu muda mrefu pia upatikanaji wa mbolea inayoweza kutumika kwa kilimo lakini tunaishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa kuwezesha ujenzi wa mradi huu”Alisema

“Sisi Tanga Uwasa tumeona ujenzi wa vyoo umekamilika na vipo tayari kutumika tunadhani hakuna haja ya kuendelea kusubiri hadi ujenzi wa miundombinu pale Kilapula ukamilike ikiwa wanafunzi na wananchi sokoni wanauhitaji mkubwa hivyo tunakuomba ukabidhi vyoo hivi kwa uongozi wa shule ya Sekondari Bonde, Shule ya Msingi Mdote na Soko la Majengo vianze kutumika na hivyo kusaidi kupunguza changamoto iliyopo ya uhitaji wa matundu ya vyoo”Alisema

Awali akizungumza mara baada ya kupokea mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Maji Taka wilayani Muheza pamoja na kukabidhi Vyoo vilivyojengwa ikiwa ni sehemu ya Ujenzi wa Mradi huo kwa shule ya Sekondari Bonde, Shule ya Msingi Mdote na Soko la Majengo wilayani Muheza, Mkuu wa wilaya ya Muheza ZainabuAbdallah alisema miaka mitatu ya nyuma hali ya upatikanaji wa maji ilikuwa ni asilimia 33 lakini miaka mitatu sasa hivi himefikia 71 hiyo ni kazi kubwa anayoifanya Rais Dkt Samia Suluhu.

Katika miaka mitatu ya Rais Dkt Samia wamefanikiwa kutekeleza miradi mikubwa ya kikamkati 20 yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 161.4 ya Maji Safi na Maji Taka miradi sita yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 4.2 ambapo hiyo ni kazi kubwa na nzuri inayofanya na Rais Samia.

Alisema wamefika katika hafla hiyo kuungana na Tanga Uwasa katika tukio hilo huku akimpongeza Waziri wa Maji Jumaa Aweso kutokana na kazi kubwa anayofanya kuhakikisha huduma ya maji kwenye mkoa wa Tanga inakuwa nzuri na Muheza wanatekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa miundombinu ya maji taka wenye thamani ya zaidi ya Bilioni 1 ambapo kwenye mradi ho wamepata gari la maji taka, gari ya usimamizi wa mradi na wamepata matundu ya vyoo,shule ya sekondari na Msingi pamoja na Soko .


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post