DKT. TULIA ASHIRIKI MKUTANO WA JUMUIYA YA MADOLA GHANA

 

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 5 Oktoba, 2023 ameshiriki Mkutano wa 66 wa Kibunge wa Jumuiya ya Madola (CPC) unaoendelea katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Accra nchini Ghana wenye dhima isemayo “The Commonwealth Charter 10 years on: Values and Principles for Parliaments to Uphold”

Katika Mkutano huo, Dkt. Tulia ameambatana na baadhi ya Wabunge akiwemo Mhe. Dkt. Alice Kaijage, Mhe. Abdallah Mwinyi, Mhe. Dkt. Pius Chaya, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama, Mhe. Elibariki Kingu pamoja na Katibu wa Bunge Bi. Nenelwa Mwihambi ndc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post