TANZANIA YAPONGEZWA KUBORESHA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI, ALJAZEERA YAAHIDI KUTOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI TZ


Mwenyekiti wa JOWUTA Mussa Juma akiwa na Mkurugenzi wa Aljazeera Sami Elhag
#Tanzania yasifiwa kuboresha Mazingira ya Kazi kwa wanahabari na viongozi wa IFJ


Na: Mwandishi wetu. Arusha

maipacarusha20@gmail.com

Shirika la Utangazaji la kimataifa la Aljazeera limekubali , kushirikiana na Chama Cha wafanyakazi katika wa Vyombo vya habari nchini (JOWUTA) kutoa mafunzo kwa wanahabari ya usalama kazini na uandishi wa habari za uchunguzi.

Makubaliano hayo yalifikiwa katika mkutano wa ndani wa wanahabari Afrika , ulioandaliwa na shirikisho la kimataifa la waandishi wa habari Afrika (IFJ) ikiwa ni mfululizo wa vikao vya pembeni vinavyoendana na Kikao cha 77 Cha Tume ya Afrika ya Haki za Binaadamu na Watu(ACHPR) ambavyo vinaendelea jijini Arusha.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Aljazeera wa masuala ya jamii na Haki za Binaadamu,Sami Elhag amesema aljazeera ipo tayari kusaidia wanahabari wa Tanzania ili kufanya kazi kwa ufanisi.

Elhag amesema miongoni mwa maeneo ambayo wataweza kusaidia ni mafunzo kwa wanahabari katika masuala ya usalama, jinsi la kuandika habari za uchunguzi lakini pia ya kuboresha Utendaji wa kazi na kubadilishana uzoefu..


Alisema wanahabari Duniani wanakabiliwa na changamoto nyingi za kiusalama na tayari kituo cha aljazeera wanahabari wake wamepatwa na changamoto mbalimbali.

Ahadi hiyo ya Aljazeera ilitolewa kutokana na maombi ya Mwenyekiti wa JOWUTA,Mussa Juma kuomba wanahabari nchini kupata fursa ya mafunzo na ziara za kubadilishana uzoefu.

Juma alisema, wanahabari wanakabiliwa na changamoto za kiusalama wakiwa kazini hasa wanapokwenda kuandika habari sehemu zenye migogoro, maslahi duni na lakini wengi hawana ujuzi wa kutosha wa uandishi wa habari za uchunguzi na Vita na kukabiliana na majanga.


Awali Katibu wa IFJ Louis Thomasi alisema wanahabari maeneo mengi Duniani wanakabiliwa na changamoto za kiusalama kazini lakini pia na uwepo wa sheria ambazo ni kandamizi.


Amesema kuna haja ya wanahabari kupatiwa mafunzo ya kiusalama lakini kupatiwa huduma muhimu ikiwepo maslahi na kuwepo sheria ambazo zitakuza Uhuru wa Vyombo vya habari na Uhuru wa kujieleza.

Thomasi alitaka Serikali barani Afrika kuwa na sheria rafiki ambazo zinasaidia wanahabari kufanya kazi vizuri na hivyo kuchangia ukuaji wa demokrasia na Maendeleo.

Awali Mwakilishi wa Shirika la kimataifa la A19, Alfred Bulakali alisema hakuna Demokrasia kwenye taifa lolote bila kuwepo Uhuru wa Vyombo vya habari na Uhuru wa kujieleza.

Bulakali alisema Uhuru wa Vyombo vya habari ni oxygen ya demokrasia hivyo ni muhimu serikali barani Afrika kutoa Uhuru kwa vyombo vya habari.


Tanzania yapongezwa kuboresha Uhuru wa Vyombo vya habari

Hata hivyo Tanzania ilipongezwa katika mkutano huo kutokana na kuendelea kuboresha Mazingira ya kufanya kazi kwa wanahabari ikiwepo kuendelea na maboresho ya sheria mbalimbali na kutoa Uhuru wa kujieleza na kukusanyika.

Akiwasilisha mada katika mkutano huo , Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari Maelezo Rodney Thadeus alisema serikali ya Tanzania imeboresha mazingira ya wanahabari kufanyakazi na Uhuru wa kujieleza.


Thadeus alisema Rais wa Tanzania,Dk Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuingia madarakani alitaka kupitiwa sheria za habari na kuboresha zoezi ambalo linaendelea vizuri.


Alisema kwa wanahabari Tanzania wamehakikishiwa Uhuru wa kufanyakazi lakini pia kwa kutokana na maboresho ya sheria makosa ya kitaaluma.yameondolewa kuwa ya kijinai,kutakuwa na baraza huru la habari na kuanzishwa Mfuko wa kusaidia wanahabari kielimu.

"Serikali inaendelea kushirikiana na wadau wa habari katika maboresho ya sheria na serikali inawahakikishia mazingira mazuri wanahabari"alisema

Akizungumza maombi ya mafunzo kwa wanahabari yaliyotolewa na JOWUTA , Thadeus alitaka mafunzo hayo kuhusisha pia maafisa habari wa Serikali.

"Suala la mafunzo na kubadilishana uzoefu linapaswa pia kuwafikia maafisa habari ambao ndio wanafanya kazi na waandishi lakini pia wengi wao ni waandishi na watangazaji ambao wanahitaji pia mafunzo",amesema.

Wakili Mary Mwita na Wakili Mgusuhi Maswi kutoka Mawakili wa Umoja wa Pan Afrika( PALU ) wakitoa mada zao walisema ni muhimu wanahabari kufanyakazi katika mazingira Salama wakiwepo Wanahabari wanawake ambao wamekuwa waathirika wa ukatili katika vyombo vya habari.


Wakili Mwita alisema, waandishi wanahabari wamekuwa wahanga wa ukatili hivyo ni muhimu kuendelea kujengewa uwezo lakini pia kuwepo na sheria ambazo zinawalinda.

Katibu wa Umoja wa waandishi wa habari nchini Kenya,(KUJ) Erick Oduor alisema ni muhimu kuwepo na muongozo katika kusimamia masuala ya Ulinzi na Usalama kwa wanahabari.


"Kenya tayari tunamuongozo na tupo tayari kushirikiana na JOWUTA na wadau wengine kuwepo na muongozo kama huo katika nchi zao ili kuboresha Utendaji kazi kwa wanahabari"alisema.

Akifunga mkutano huo Mwenyekiti wa JOWUTA Taifa ,Mussa Juma aliwapongeza wanahabari kutoka nchi mbalimbali kushiriki mkutano huo na kuwahakikishia watafurahi amani na Utulivu wa Tanzania.


"Mkutano wetu umekuwa mzuri sana tumejadiliana mambo muhimu kuboresha sekta ya habari Afrika lakini kubwa zaidi nashukuru Aljazeera kukubali kuja kusaidia wanahabari wa Tanzania"alisema.


Juma alipongeza serikali ya Tanzania kwa kuboresha Mazingira ya wanahabari kufanyakazi tofauti na nchi nyingine na kuahidi JOWUTA itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wa habari kuhakikisha wanahabari wanafanya kazi katika mazingira Salama.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post