DKT. KIDA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KUSHIRIKI MKUTANO WA BIASHARA NA UWEKEZAJI WA EAC

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji Dkt. Tausi Kida ameongoza ujumbe wa Serikali ya Tanzania kushiriki Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Biashara na Uwekezaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi ya Marekani.

Mkutano huo umefanyika Julai 18, 2023 nchini Kenya ambapo Dkt. Kida amemwakilisha Waziri wa Ofisi hiyo Prof. Kitila Mkumbo ambapo Marekani na Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zimejadili namna ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja za biashara na kuvutia uwekezaji.

Aidha, wamejadiliana kutumia kikamilifu fursa za soko la mpango wa AGOA nchini Marekani, Mkataba wa eneo huru la biashara Afrika (AfCFTA) na mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Wengine waliohudhuria mkutano huo ni Mwakilishi wa Biashara wa Serikali ya Marekani Mhe. Balozi Katherine Tai, Mawaziri wa Biashara na Uwekezaji wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na sekta binafsi ya Tanzania imewakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) Raphael Maganga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post