Tazama picha : CHIMBO JIPYA LA BURUDANI 'A2C BAR & GRILL' JIJINI MWANZA

Baada ya miaka mingi kupita lile chimbo lako la kijanja kufungwa The Kiss lililopo Kirumba Mwanza, sasa kiota hiki cha wapenda burudani Rock city kipo hatua za mwisho kukamilika.


The Kiss ya zamani kwa sasa itajulikana kama A2C Bar & Grill, ambapo eneo hilo la kijanja kama linavyoonekana kwenye picha, vinywaji na chakula kitamu vitauzwa huku mziki mzuri ukisindikiza siku yako.


Kwa mjibu wa Mkurugenzi wa A2C, Benedict Mara, amesema chimbo hilo la kijanja lipo hatua za mwisho kukamilika na uzinduzi unaotarajiwa kufanyika Julai 13,2023 (siku ya Ijumaa)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post