MKULIMA APIGWA RISASI


Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Walter Kaaya (34) mkazi wa Simanjiro mkoani Manyara amenusurika kifo kwa kupigwa risasi na Paulo Laizer (43) mfugaji wilayani humo kufuatia mzozo wa mifugo kukutwa shambani ikiharibu mazao.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara RPC George Katabazi amesema majeruhi alikuwa akiondoa ng'ombe hizo kwenye shamba lake la ekari 200 zilizokuwa na mazao mbalimbali yakiweno mahindi na maharagwe

Wakati anaziondoa ng'ombe shambani mtuhumiwa alifika na kuibua mzozo na kuchukua silaha yake aina ya bastola na kumpiga risasi begani

Majeruhi amekimbizwa katika hospitali ya KCMC Moshi kwa matibabu zaidi.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post