Tanzia : MMILIKI WA KAMPUNI YA NDEGE YA PRECISION AIR AFARIKI DUNIA


Taarifa za kuhuzunisha zilizotufikia kwenye chumba chetu cha habari zimeeleza kuwa, mmiliki wa Kampuni ya Ndege ya Precision Air, Michael Ngaleku Shirima amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80.

Taarifa hizo zimeeleza kuwa, Mzee Shirima amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Juni 10, 2023 alipokuwa akipatiwa matibabu hospitalini jijini Dar es salaam.

Imeelezwa kwamba Mzee Shirima alilazwa hospitalini tangu Juni 8, 2023.

Kifo cha Mzee Shirima kimethibitishwa na Kampuni ya Precision Air.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post