SERIKALI YAANIKA SABABU ZA KUICHAGUA KAMPUNI YA DP WORLD YA DUBAI KUENDESHA BANDARI

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa ameeleza sababu za Serikali kuichagua kampuni ya DP World ya Dubai kuja kuendesha Bandari ya Dar es Salaam, ikiwa ni pamoja na uzoefu wa kampuni hiyo katika kazi.


Profesa Mbarawa amebainisha hayo leo Jumamosi Juni 7, 2023 wakati akitoa maelezo ya awali bungeni yakihusu mapendekezo ya kuridhia mkataba baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kuhusu ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa ajili ya uendelezaji na uboreshaji wa utendaji kazi wa bandari Tanzania.


Amesema kutokana na changamoto za bandari zilizopo na kwa kuzingatia dhima ya Serikali ya kuboresha sekta ya bandari nchini ili kuongeza ufanisi na mchango wake katika mapato ya nchi, ajira na kuchagiza sekta nyingine za kiuchumi; Serikali ilifanya uamuzi wa kutafuta wawekezaji wapya wanaoendana na dhima ya Serikali.

Chanzo - Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments