KAMATI YA BUNGE YASHAURI MIKATABA ITAKAYOSAINIWA ITAJE MUDA MAALUMU WA UTEKELEZAJI


Kamati ya Bunge ya Miundombinu imeshauri mikataba ya utekelezaji itakayosainiwa itaje muda maalumu wa utekelezaji wa miradi ambao utazingatia maslahi mapana ya nchi ya Tanzania.


Ushauri huo umetolewa leo Jumamosi Juni 10, 2023 bungeni Dodoma na mwenyekiti wa kamati hiyo, Selemani Kakoso wakati akitoa maoni ya kamati kuhusu azimio la Bunge kuridhia makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kuhusu ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa ajili ya uendelezaji na uboreshaji wa utendaji kazi wa bandari Tanzania.


“Kamati inasisitiza kwamba uhai wa mikataba ya utekelezaji itakayosainiwa itaje muda maalumu wa utekelezaji wa miradi ambao utazingatia maslahi mapana ya nchi.

Chanzo - Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments