SERIKALI YARIDHIA KUONGEZWA MUDA WA TATHMINI YA HALI YA VYOMBO VYA HABARI NCHINI



Na Dotto Kwilasa,Dodoma.

SERIKALI kupitia Wizara ya Habari Mawasiliano na teknolojia ya Habari,imeridhia kuiongezea muda wa miezi sita  Kamati ya Tathmini ya hali ya uchumi kwa Vyombo vya Habari na Wanahabari nchini  ili iweze kufanya kazi yake kwa ufanisi zaidi.

Waziri wa Habari,Mawasiliano na teknolojia ya Habari,Nape Nauye ametoa kauli hiyo leo Mei 23,2023 Jijini Dodoma mara baada ya Kukutana na Kamati hiyo huku ikiomba kuongezewa muda huo kutokana na kazi waliyopewa  kuhitaji utafiti wa kina na waki taalam  na muda wa miezi mitatu ambao walipewa awali kutotosha.

Katika hatua nyingine Waziri Nape ametoa wito kwa wadaiwa wote   ambao wanadaiwa na Vyombo mbalimbali vya Habari  hapa nchini kulipa madeni hayo.

Amesema tathimini ya hali ya uchumi wa vyombo vya habari nchini inatarajiwa kutolewa mwezi Novemba mwaka huu, huku serikali ikiwata waandishi wa habari pamoja na wadau wa tasnia hiyo kutoa ushirikiano kwa kamati husika ili kunuru vyombo vya habari nchini.

“Nimekutaka na Kamati hii awali tulikuwa tumeipa miezi mitatu lakini kutokana na umuhimu wa tasnia hii na maagizo ya Mheshimiwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan ameagiza kuwa jambo hili lisifanywe kwa kuhalakishwa bali lifanywe kwa umakini wa hali ya juu ili kuleta mabadiliko katika tasnia hii”amesema Nape

Waziri huyo, amesema kamati hiyo badala ya kuharakisha jambo hilo inapaswa kufanya tafiti za kina kwa kuhusisha wadau wengi ili kupata maoni ambayo yatakuwa na manufaa na vyombo vya habari nchini.

“Jambo hili linasubiriwa sana na dunia watu wanataka kuona nini Tanzania inakwenda kufanya katika kuleta mageuzi kwenye tasnia hii ya vyombo vya habari nchini hivyo lazima tuje na kitu kinacholeta mabadilko kwa vyombo vyetu vya habari nchini”amesema

Amesema hadi sasa anaridhishwa na kazi ambayo inaendelea kufanywa na kamati hiyo kutokana na kushirikisha wataalam kutoka  nyanja mbalimbali ambao wameongeza tija katika tathimini hiyo.

“Kutokana na ramani ambayo kamati hii imeichora hadi sasa inaonyesha ni kwa jinsi gani inakwenda kuleta mambo ambayo yatakwenda kujibu changamoto mbalimbali zinazo ikabili sekta hii ya habari.

“Hivyo basi nitowe wito kwa waandishi wa habari na wadau wengine wa habari nchini kutoa ushirikiano kwa kamati hii ili ifanikishe jambo hili na kuleta mabadiliko kwenye vyombo vya habari ambavyo vingi hivi sasa vipo hoi”amesema Nape

Katika nyingine waziri hiyo wa Habari amesema wakati jambo hilo likiendele mchakato wa sheria ya vyombo vya habari pamoja na sera utaendelea na kama itaoneka ipo haja kufanyiwa maboresho yatafanywa.

Awali Mwenyekiti wa Kamati ya kutathmini  hali ya uchumi kwa Vyombo vya Habarai na wanahabari,Tido Mhando  ameomba Serikali kuwaongezea muda kutokana na kazi hiyo kuhitaji utafiti wa kitaalam  zaidi.


Amesema kuwa yeye pamoja na wajumbe wote wamelivalia njuga suala hilo ili kusaidia vyombo vya habari na wanahabari nchini.

Kadhalika, Mhando amesema watahakikisha jambo hilo linakamilika ifikapo mwezi Novemba mwaka huu kwa mujibu wa muongozo waliopewa ili kulisaidia taifa.

“Matatizo ya vyombo vya habari yapo sehemu nyingi duniani inasikitisha sana kuona wanahabari nchini kuendelea kuwa ombaomba na kutegemea bahasha ili waishi na kutokuwa na uhakika wa kesho yao”alisisitiza Mhando.

Kamati hiyo iliundwa rasmi Januari 23 Mwaka huu ikiwa na Wajumbe tisa  ikiongozwa na Mwenyekiti wake Tido Mhando na Katibu ni Gerson Msigwa ambayo  inatarajiwa kukamilisha kazi yake mnamo Mwezi  Novemba Mwaka huu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments