MAAFISA UTAMADUNI ZANZIBAR WAPIGWA MSASA KUONGEZA UFANISI


Maafisa Utamaduni wa Wilaya za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wamepatiwa mafunzo ya kuimarisha Utendaji wao katika kukuza Sekta ya Utamaduni katika maeneo yao ya kazi.

Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku tatu kuanzia Aprili 14 hadi 16 Mjini Bagamoyo na yatahusisha mada mbalimbali chini ya Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni Dkt. Emmanuel Temu.

Miongoni mwa mada zilizowasilishwa kwa siku ya Aprili 14, 2023 ni pamoja na Majukumu ya Maafisa Utamaduni Kisera na Kimundo, Uhifadhi na Uendelezaji wa Urithi wa Utamaduni pamoja na Uhifadhi na Uendelezaji wa Urithi wa Bara la Afrika.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments