MALUNDE ASHINDA TUZO YA MTU BORA WA VYOMBO VYA HABARI 2022/2023 'BEST MEDIA PERSONALITY AWARD'


Mkurugenzi wa Mtandao Maarufu wa Malunde 1 blog www.malunde.com ndugu Kadama Malunde ametangazwa kuwa mshindi wa Tuzo ya Mtu Bora wa Vyombo vya Habari Shinyanga 'Best Media Personality Awards 2022/2023' zilizoandaliwa na Taasisi ya Holysmile ambayo ni inatoa huduma za Sanaa, Utamaduni na Burudani pamoja na kutambua na kuthamini juhudi na harakati zinazofanywa na wadau wote wa maendeleo iliyosajiliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Kadama Malunde, ambaye ni Mwandishi wa Habari Mkoani Shinyanga ametangazwa Mshindi Mtu Bora wa vyombo vya habari 2022/2023/ Mtu Bora wa Vyombo vya Habari/Best Media Personality/ Mwandishi wa Habari Mwenye Mvuto na Ushawishi katika Media wakati wa tamasha la utoaji tuzo (SHINYANGA MDAU SHUPAVU AWARDS) lililofanyika Machi 31,2023 Mjini Shinyanga.
 


 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments