YESU WA TONGAREN AGOMA KUSULUBISHWA


Eliud Wekesa almaarufu yesu wa Tongaren kutoka kaunti ya Bungoma nchini Kenya ameonekana kuwajibu watu waliotaka asulubishwe wakati huu wa pasaka jinsi Yesu Kristo alivyofanyiwa.

Katika Video iliyosambazwa mtandaoni yesu wa Tongaren anasikika akisema kuwa katika maandiko yake na kuelewa kwake kwa kitabu kitakatifu hakuna mahali ambapo yesu alisulubishwa mara mbili.

"Sijawahi kuona mahali popote hata katika chuo changu cha mbinguni kwamba waliandika yesu atasulubiwa mara ya pili," Yesu wa Tongaren alisema. 

Yesu wa Tongaren alisema kuwa imeandikwa kuwa yesu atakaporudi atakuwa sawa na bali hatorejelea tena katika usulubissho aliopitia kuwakomboa wanadamu.

Yesu wa Tongaren ameongoza ibada ya maombi ya siku kuu ya pasaka katika kanisa lake na kusema kuwa watafunga kwa kwa siku tatu wakiomba.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post