BINGWA WA DUNIA WA BAISKELI ATAKA KUINGIA REKODI YA GUINESS KUPITIA MLIMA KILIMANJARO



Bingwa wa Kuendesha Baiskeli Duniani mara 5 mfululizo kutoka Poland Mike "Leszek" Mikulski @mikelmikulski ambaye yuko katika maandalizi kabambe ya kuweka rekodi ya Dunia ya Guiness kwa kupanda Mlima Kilimanjaro kwa baiskeli akitumia saa chache zaidi kuliko mwanadamu yeyote, leo amekutana na viongozi wa Wizara ya Utalii nchini katika kuona namna tukio hilo linavyoweza kuileta dunia hapa Tanzania.

Inakadiriwa zaidi ya watu 200, wakiwemo wanahabari wa kimataifa na majaji kutoka Kamati ya Dunia ya Guiness, watafuatana naye kuja nchini kushuhudia na kuithibitisha rekodi hiyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post