YANGA SC YATOKA SARE UGENINI DHIDI YA REAL BAMAKO



KLABU ya Yanga imelazimishwa sare ya bao 1-1 na timu ya Real Bamako kwenye hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kufanikiwa kuichapa Real Bamako bao 1-0.

Katika mchezo huo, Yanga haikuweza kucheza mpira mzuri kipindi cha kwanza kwani hawakutengeneza nafasi kwenye lango la upinzani mpaka mapumziko ambako timu zilienda zikiwa hazijapata bao.

Kipindi cha pili timu zote ziliingia zikihitaji bao kwani ziliweza kutengeneza nyingi licha ya Yanga kutumia vizuri nafasi moja na kuweza kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wao hatari Fiston Kalala Mayele ambaye alipokea pasi kutoka kwa Aziz Ki.

Real Bamako katika dakika za lala salama waliweza kupata bao la kusawazisha kupitia kona ambayo ilizaa bao.

Yanga Sc sasa itakuwa inashika nafasi ya tatu kwenye kundi lao wakiwa wamecheza mechi tatu na kujikusanyia pointi nne ikiwa anaeongoza Monastir akiwa na pointi saba.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments