YANGA SC YAICHAPA TP MAZEMBE 3-1, YAONDOKA NA MILIONI 15 ZA MAMA


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM 

KLABU ya Yanga imefanikiwa kuondoka na alama tatu mbele ya timu ya TP MAzembe ya nchini DR Congo baada ya kuichapa kwa mabao 3-1 kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.

 Yanga katika mchezo huo waliweza kutawala katika kipindi cha kwanza ambapo walifanikiwa kupata mabao mawili ya haraka kupitia kwa nyota wao Kennedy Musonda dakika 7 na Mudathir Yahaya kufunga dakika ya 11. 

Kipindi cha pili Yanga walirudi wakiwa wanajiamini hivyo kuwafanya TP Mazembe wachezee mpira na kufanikiwa kupata bao kupitia kwa Alex Ngonga aliepiga mpira wa adhabu na kutinga nyavuni.

 Bao la tatu limefungwa na Tusila Kisinda dakika ya 91 ya mchezo baada ya kuingia akitokea benchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments