WALIOFARIKI TETEMEKO LA ARDHI UTURUKI NI ZAIDI YA 8,700


Zaidi ya watu 8,700 wanadaiwa kufariki nchini Uturuki na Syria kufuatia tetemeko la ardhi la Jumatatu. Idadi ya vifo nchini Uturuki imeongezeka hadi 6,234, kwa mujibu wa shirika la maafa nchini humo.

Ni vigumu kuthibitisha idadi hiyo nchini Syria, lakini vyombo vya habari vya serikali vinasema takriban watu 2,500 wameuawa.

Kundi la uokoaji la White Helmet, ambalo linahudumu katika eneo linalodhibitiwa na waasi, linasema idadi ya waliouawa imeongezeka hadi zaidi ya 1,280.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments