ANAYEDAIWA KUWA MWIZI ANUSURIKA KUUAWA BAADA YA KUDAKWA NA BATA TAMBUKARELI SHINYANGA MJINI

Kijana aliyejulikana kwa jina Musa amenusurika kuuawa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira kali katika eneo la Tambukateli kata ya Ndembezi Mjini Shinyanga baada ya kukamatwa na bata anayedaiwa kumuiba katika mtaa huo huku mwenyewe akikiri kufanya matukio ya wizi katika eneo hilo.


Tukio hilo limetokea majira ya sita mchana leo Jumanne Januari 2,2023 ambapo wananchi wenye hasira wamemshambulia kijana huyo kabla ya askari polisi kufika eneo la tukio na kumuokoa kijana huyo.

Wakati hayo yanajiri mkazi wa eneo hilo ambaye hatukufanikiwa kupata jina lake naye anaugulia maumivu baada ya kupewa kichapo wakati akizuiwa asimpige mtuhumiwa huyo wa wizi.


Mtuhumiwa wa wizi akiwa na bata pembeni


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments