MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI MSISHA AUAWA KWA KUKATWA MAPANGA

Mwanafunzi wa darasa la sita katika shule ya Msingi Msisha halmashauri ya wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera Joyce Exavery (13) ameuawa kwa kukatwa mapanga  akiwa nyumbani kwao katika kijiji cha Ruhita kata ya Kamuli.


Tukio hilo limetokea jana mchana Jumapili Desemba 25,2022 ambapo inaelezwa kuwa mwanafunzi huyo alifanyiwa ukatili (kuchinjwa) na mtu/watu ambao bado hawajafahamika.

Kamanda wa Polisi wa Kagera William Mwampagale amethibitisha kutokea kwa tukio hilo akizungumza na Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments