NAIBU WAZIRI KATAMBI AONGOZA KIKAO KAZI CHA TATHMINI NA MIKAKATI YA UTEKELEZAJI MAJUKUMU OFISI YA WAZIRI MKUU

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi amekutana na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya ofisi hiyo hii leo tarehe 23 Disemba, 2022 katika jengo la OSHA, jijini Dodoma. 

Lengo la kikao kazi hicho ni kufanya tathmini na kupanga mikakati ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi hiyo.

Akizungumza na menejimenti ya Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mheshimiwa Katambi amewataka viongozi hao kuendelea kuchapa kazi kwa bidii, ufanisi, kushirikiana na kuwa wabunifu katika kutekeleza majukumu yao ili kufikia matarajio ya Serikali na wananchi wanaowahudumia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments