YANGA HAIKAMATIKI, YASHINDA TENA 2-0 MBELE YA MBEYA CITY



***********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

KLABU ya Yanga imeendelea kujiweka vizuri kwenye msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara mara baada ya kufanikiwa kuichapa Mbeya City mabao 2-0 na kuwafanya kufika pointi 32 akiwa ameshuka dimbani mara 12.

Fiston Kalala Mayele ameendelea kutikisa nyavu baada ya leo tena kupachika mabao mawili na kumfanya aendelea kushikilia usukani kwa wapachikaji wa mabao ndani ya ligi kuu akifikisha mabao 10.

Bao la kwanza Mayele alifunga dakika 24 ya mchezo kipindi cha kwanza na bao la pili akifunga dakika 79 kipindi cha pili.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments